MZIMU WA MOURINHO UNAENDELEA KUMTESA VAN GAAL

Van Gaal +Mourinho src="http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/02/Van-Gaal-Mourinho.jpg" width="640" />


Kocha wa Manchester United mholanzi Louis Van Gaal jana ameendeleza vita yake na waandishi wa habari nchini England baada ya kuulizwa swali kuhusu ujio wa Jose Mourinho Old Trafford
Van Gaal alikasirishwa na swali aliloulizwa na mwandishi mmoja wa habari kuwa kiwango kizuri kinachooneshwa na timu yake kwa sasa ni kwa sababu kuwa klabu inajiandaa kumtangza mrithi wake?
Akiwa katika hali ya hasira baada ya timu yake kulazimishwa sare ya goli 1-1 dhidi ya Chelsea, asante kwa goli la Diego Costa katika dakika za lala salama Van Gaal alikuwa na haya ya akujibu
“Mmeshaongea na Ed Woodward? alisema. Kwanini wakatae (tetesi kuhusu Mourinho?) siingilii pia. Sasa kwanini klabu ikatae kuhusu hilo. Wakati mnatengeneza habari?”
“Sawa. kwahiyo hamkuongea na Ed Woodward, na hamkuongea na familia ya Glazers pia kwahiyo mmetengeneza habari. Halafu mnataka mimi nijibu hili swali. Sijibu hili swali. Na ntarudia kila wiki “.
“Sasa labda niseme kuwa wote mnafukuzwa kesho. Mnaitwa kina nani? halafu natangaza majina yenu. Waangalieni wake zenu au watoto wenu au binamu zenu na watu wengine kama hao”.
Kwa sasa Van Gaal yupo katika wakati mgumu kutokana na timu yake ya Manchester United kutocheza na kupata matokeo mazuri kama inavyotarajiwa na mashabiki wake huku idadi kubwa ya mashabiki pamoja na wachezaji wa zamani wa Klabu hiyo wakitaka Van Gaal atimuliwe katika kiti hicho cha Old Trafford

Comments

Popular posts from this blog

WANAOWANIA KUPANDA LIGI KUU BARA HAWA HAPA, KAZI IPO JUMAMOSI

AIBU!!! MIMBA YAMUUMBUA WEMA SEPETU

South Korea, U.S. begin exercises as North Korea threatens attack